Kijana
Said ambaye aliteseka na uvimbe mkubwa usoni sasa amepona baada ya
kufanyiwa upasuaji katika Hospital ya CCBRT iliyopo jijini Dar.
Akizungumza na waandishi wa habari hii, Ngawaje alisema kwa sasa ana
amani moyoni na kuhisi raha ya dunia baada ya kuteseka kwa muda mrefu
huku akiamini hawezi kupona tena.“Mimi siamini kama ule mzigo mzito
uliokuwa umefunika usoni wangu haupo, nilikuwa nashindwa kulala kwa
mawazo, sasa hivi niko sawa,”
alisema.Ngawaje
alisema matunda hayo ameyapata baada ya gazeti hili la Machi 11, mwaka
huu kutoa habari yake ukurasa wa 15 akielezea matatizo yake, watu
mbalimbali walimchangia fedha kwa ajili ya matibabu.
INGAWAJE
Said (38), mkazi wa Bagamoyo kwa Mtoro, Pwani ambaye aliteseka na uvimbe
mkubwa usoni kwa miaka 12 sasa amepona baada ya kufanyiwa upasuaji
katika Hospital ya CCBRT iliyopo jijini Dar.
Muonekano
wa uvimbe aliokuwa nao kabla ya kufanyiwa upasuaji. “Halafu akajitokeza
mfadhili mmoja ambaye alitoa fedha zote za kufanyiwa upasuaji ambapo
upasuaji wa kwanza alifanyika Julai 15, mwaka huu na wa pili Oktoba 30,
mwaka huu.
Post a Comment