Putin aondoka katika mkutano wa G20
Rais wa Urusi Vladimir Putin alikuwa kiongozi wa kwanza kuondoka
katika mkutano wa kilele wa kundi la nchi 20 zenye nguvu kubwa
kiuchumi unaoendelea nchini Australia, wakati viongozi wenzake
wakijitayarisha kuzindua mpango wao wa kuimarisha uchumi duniani.
Putin alikosolewa vikali na viongozi wenzake wa Ulaya kutokana na
hatua yake, ya kuingilia mgogoro wa Ukraine. Kati ya waliomkosoa ni
pamoja na Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron na Kansela
wa Ujerumani Angela Merkel aliyesema huenda Urusi ikawekewa
vikwazo zaidi. Suala muhimu katika mkutano huo wa G20 hii leo ni
mipango ya kuchochea ukuaji wa uchumi kwa asilimia 2 ifikapo
mwaka 2018 hali inayoweza kuongeza nafasi za kazi na kuinua
uchumi duniani. Kwa upande mwengine Katibu Mkuu wa Umoja wa
Mataifa Ban Ki Moon ameyatolea mwito mataifa ya kundi la G20
kushirikiana kudhibiti mabadiliko ya tabia nchi na kuchangia katika
mfuko wa fedha utakaoyawezesha mataifa yanayoendelea
kupambana na mabadiliko ya tabia nchi.
Post a Comment