0
Kansela wa Ujerumani Angela Merkel amewasili mjini Sydney Australia hii leo katika siku ya mwisho ya ziara yake nchini New Zealand na Australia. Merkel anatarajiwa kuwa na mazungumzo na Waziri Mkuu wa Australia Tony Abbot  juu ya uhusiano kati ya nchi hizo mbili. Ziara ya mwisho nchini Australia ilifanywa na Kansela wa Ujerumani  Helmut Kohl mnamo mwaka wa 1997. Katika ziara hii Kansela Angela Merkel siku ya Jumatatu atakutana na kiongozi wa Upinzani wa chama cha Labour nchini Australia Bill Shorten kabla ya kurejea Ujerumani. Australia ni mshirika muhimu wa kimkakati wa Ujerumani katika kanda ya Asia na Pacific wakati Ujerumani ni mfanyabiashara muhimu barani Ulaya kwa Australia baada ya Uingereza.

Post a Comment

 
Top