0

Alex Song released a statement on his Instagram page detailing the reasons for his decision  

Kiungo raia wa Cameroon anayekipiga kwa mkopo kwenye klabu ya West Ham United akitokea klabu ya Barcelona ya nchini Hispania Alex Song ametangaza kupitia mtandao wake wa tweeter kuwa ameamua kujiuzuru kuitumikia timu yake ya taifa.

Song shields the ball from Alex Oxlade-Chamberlain during West Ham's clash with Arsenal in December  
Song ameonekana kutoridhishwa na kitendo cha mara kadhaa kutemwa kwenye kikosi cha timu hiyo ya taifa na hivyo kuamua kujiweka pembeni ili awapishe wachezaji chipukizi waoneshe uwezo wao.
 Song will be returning home from Cameroon in time for West Ham's match against Swansea City on Saturday
" Tangu kumalizika kwa michuano ya kombe la Dunia kule nchini Brazil kumekuwa na hali ya mimi kuachwa kwenye kikosi cha timu ya taifa mara kadhaa, Lakini kubwa zaidi ni hili la mimi kuachwa kwenye kikosi cha timu ya taifa kwaajili ya michuano mikubwa kabisa ya Afrika inayotarajiwa kushika kasi mwaka huu."

Referee Pedro Proenca from Portugal gives a red card to Cameroon's  Song during the 2014 World Cup 
"Kumekuwa na mazungumzo baina ya chama cha soka ma meneja wa timu ya taifa ili niweze kujumuishwa kwenye kikosi hicho lakini mimi binafsi nimeonelea ni bora nikae pembeni kulikoni kulazimisha jambo ambalo meneja wa timu ya taifa linalotazamwa na watu wengi zaidi halitaki."

"Nafahamu kuwa ni mapema sana kwa mchezaji wa umri wangu kutangaza najiuzuru kuitumikia timu yangu ya taifa na mimi binafsi najisikia vibaya sana kwa jinsi hali ya mambo yanavyokwenda lakini nitafanya nini na mazingira ndio yako hivyo ambavyo tumeyaona

Post a Comment

 
Top