0
Tanzania Sanjari Na nchi Nyingine Duniani Kuadhimisha Siku Ya Ukimwi
Tanzania ikiungana  na nchi nyingine Duniani hii leo kwenye kilele cha maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani,Serikali kupitia wizara ya afya imesema  kiwango cha maambukizi ya virusi vya ukimwi kimepungua kutoka asilimia 18 miaka ya nyuma  hadi asilimia 5.3 kwa sasa
Akizungumza na radio kili Fm, Katibu Mkuu  wa wizara ya afya na ustawi wa jamii,  Dkt Donald Mbando amesema  kiwango hicho kimepungua kutokana na uanzishwaji wa dawa za kufubaza makali ya Virusi vya ukimwi mapema kwa watu wanaoishi na maambukuzi ya virusi hivyo
Bado elimu ya unyanyapaa kwa jamii haijafanikiwa kwa kiwango stahiki kutokana na mienendo ya kuwatenga  watu wanaoishi na virusi vya ukimwi na kutopatiwa  msaada na jamii inayowazunguka hali inayowafanya wajihisi wanyonge ndani ya jamii.
Maadhimisho ya Siku ya ukimwi Duniani kitaifa  mwaka huu yanafanyika   Mkoani Njombe
Kauli mbiu ya siku ya ukimwi duniani mwaka huu ni “Tanzania bila maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi,Vifo vitokanavyo na Ukimwi na Ubaguzi pamoja na unyanyapaa, Inawezekana.”

Post a Comment

 
Top