Lake amesema kuwa kadhalika mtoto mwingine alifariki dunia baada ya bomu kumlipukia kifuani huko Maiduguri. Mkuu huyo wa UNICEF ameitaka jumuiya ya kimataifa kutosahau kuwa bado watoto zaidi ya 200 ambao walitekwa nyara na kundi la kigaidi la Boko Haram hawajapatikana. Lake amesema, maneno matupu hayatoshi kuelezea hasira dhidi ya vitendo hivyo wala kupunguza uchungu wa madhila hayo ya kaskazini mwa Nigeria na kusisitiza kuwa taswira za hivi karibuni nchini humo na athari zake kwa mustakabali wa taifa hilo zinahitaji hatua za haraka.
UNICEF: Machafuko Nigeria yamewaathiri watoto
Lake amesema kuwa kadhalika mtoto mwingine alifariki dunia baada ya bomu kumlipukia kifuani huko Maiduguri. Mkuu huyo wa UNICEF ameitaka jumuiya ya kimataifa kutosahau kuwa bado watoto zaidi ya 200 ambao walitekwa nyara na kundi la kigaidi la Boko Haram hawajapatikana. Lake amesema, maneno matupu hayatoshi kuelezea hasira dhidi ya vitendo hivyo wala kupunguza uchungu wa madhila hayo ya kaskazini mwa Nigeria na kusisitiza kuwa taswira za hivi karibuni nchini humo na athari zake kwa mustakabali wa taifa hilo zinahitaji hatua za haraka.
Post a Comment