Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania
amekanusha wazo la baadhi ya watu kuwa nchi yake haiko tayari kupambana
na makundi yenye silaha ambayo yamesababisha hali mbaya ya usalama
nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC.
Kwenye mazungumzo kati yake na waziri wa ulinzi wa Afrika Kusini
Bw. Novisise Mapisa-Nqakula, rais Kikwete ameeleza msimamo wa Tanzania
kuwa itaendelea kujiunga na vikosi kutoka Afrika Kusini na Malawi chini
ya Tume ya kulinda amani ya Umoja wa Mataifa ili kuondoa makundi yenye
silaha nchini DRC.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment