
Moja ya watu walioweka comment zao baada ya kuiona video hii amesema hivi; “…Anyway, tusimhukumu mara zote kwenye njia negative kutokana na namna tulivyomzoea, huenda hakuwa kwenye mood…“
Kitendo alichokifanya staa wa Muziki Marekani Rihanna alipokuwa akitoka katika onyesho la mavazi 2014 British Fashion Awards kinaweza
kikamgharimu kwenye kurasa za magazeti ya udaku duniani baada ya
kumpiga mpiga picha aliyekuwa busy kumpiga picha staa huyo wakati
anatembea kutoka nje ya ukumbi lilipofanyika onyesho hilo.
The BadgalRiri alikuwa anaelekea kwenye
gari yake na hakuonekana kama alifurahishwa na mapaparazzi hao kumzonga
mbele, hivyo akafanya maamuzi ya kumpiga mpiga picha mmoja.
Wapo wanaotafsiri kitendo hicho kama
hasira na wengine wanadhani huenda hakuwa kwenye mood poa kukutana na
flashlight ya kamera kwa wakati huo.
Hii ni post yake ya mwisho kwenye
ukurasa wake wa Instagram, ukiitazama utapata jibu mtu wangu kama ile
ngumi ni bahati mbaya au makusudi.

Post a Comment